Nafasi za Kazi za Mkataba โ€“ Halmashauri ya Wilaya ya Liwale

Idara: Afya
Muda wa Mkataba: Miezi sita
Mwisho wa Kutuma Maombi: 20 Mei 2025, saa 3:30 Asubuhi
Mahali: Wilaya ya Liwale


๐Ÿง‘โ€โš•๏ธ 1. Afisa Muuguzi Msaidizi Daraja la II (ANO)

Idadi ya Nafasi: 15

Majukumu:

  • Kutoa huduma za uuguzi
  • Kukusanya takwimu muhimu za afya
  • Kuelekeza kazi wauguzi walio chini yake
  • Kutoa elimu kwa jamii kuhusu matatizo ya kiafya
  • Kutoa huduma za uzazi na kinga
  • Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake

Sifa za Muombaji:

  • Awe na Stashahada (Diploma) ya Uuguzi kutoka chuo kinachotambulika
  • Leseni ya Uuguzi na usajili kutoka Baraza la Wauguzi na Wakunga Tanzania

Mshahara:

  • Kwa mujibu wa TGHS B

๐Ÿ’Š 2. Mtenkolojia Msaidizi โ€“ Dawa

Idadi ya Nafasi: 2

Majukumu:

  • Kuandaa mahitaji ya dawa na vifaa tiba
  • Kuagiza, kuhifadhi na kugawa dawa na vifaa tiba
  • Kuandaa taarifa za matumizi ya dawa
  • Kutunza kumbukumbu za dawa na vifaa tiba
  • Kufanya kazi nyingine atakazopangiwa na mkuu wake

Sifa za Muombaji:

  • Kidato cha nne na mafunzo ya mwaka mmoja kwenye fani ya afya ya dawa

Mshahara:

  • Kwa mujibu wa TGHS A

๐Ÿฉบ 3. Daktari Daraja la II (MO)

Idadi ya Nafasi: 1

Majukumu:

  • Kutoa tiba kwa wagonjwa wa kawaida na dharura
  • Kusimamia elimu ya afya na huduma za tiba
  • Kudhibiti milipuko na kuandaa takwimu za afya
  • Kufanya tathmini za huduma za afya
  • Kuandaa mipango ya bajeti na huduma
  • Kutoa huduma za outreach
  • Kufanya kazi nyingine yoyote atakazopangiwa na mkuu wake

Sifa za Muombaji:

  • Shahada ya Udaktari kutoka chuo kinachotambulika
  • Umehitimu mafunzo ya “Internship” ya mwaka mmoja
  • Usajili wa Baraza la Madaktari Tanzania

Mshahara:

  • Kwa mujibu wa TGHS E

๐Ÿ“Œ Masharti kwa Waombaji Wote

  • Raia wa Tanzania
  • Umri: Miaka 18 hadi 45
  • Waambatishe vyeti vya kitaaluma, cheti cha kuzaliwa na CV
  • CV ijumuishe majina na namba za simu za wadhamini watatu
  • Picha moja ya “passport size” ya hivi karibuni
  • “Testimonials”, “Provisional results” na matokeo ya kidato cha IV hadi VI hayatakubaliwa
  • Barua ya maombi iandikwe kwa Kiswahili au Kiingereza
  • Barua za maombi ziwasilishwe kabla ya tarehe 20 Mei 2025, saa 3:30 asubuhi

๐Ÿ“ฌ Jinsi ya Kutuma Maombi

Tuma kwa njia ya Posta au Email:
๐Ÿ“ฎ S.L.P 23, Liwale
๐Ÿ“ง [email protected]


To apply for this job email your details to ded@liwaledc.go.tz

Related Jobs